|
Baada ya kupata Uhuru Chama cha TANU kwa kupitia
Serikali ya awamu ya kwanza ikiweka azimio la kufufua
michezo ya jadi. Kukaundwa Chama cha Michezo ya
Jadi cha Taifa (CHAMIJATA) mwaka 1976.
Mashindano ya kwanza ya Taifa yalifanyika Dodoma
mwaka 1975.
Michezo iliyoshindiwa ilikuwa mieleka, kutupa mikuki,
kulenga kwa mishale na bao.
Chama cha Michezo ya Jadi Mkoa wa Dar es Salaam
(CHAMIJADA), kilichoanzishwa na Rais wa kwanza wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Baba wa Taifa Hayati
Mwl J.K Nyerere, kimedhamiria kuufufua, kuukuza na
kuuendeleza Michezo wa Bao kufikia hatua ya kuwa
Mchezo wa Kitaifa na alama ya Taifa letu hatimaye
kuwa moja ya Michezo ya Kimataifa.
CHAMIJADA ni chama kinachosimamia na kuratibu
shughuli zote za michezo ya jadi mkoani Dar es Salaam,
ni chama halali ambacho kinaendesha shughuli zake
kisheria, kimesajailiwa kwa mujibu wa sheria ya
Baraza la Michezo la Taifa (NSC) kifungu namba 12
ya mwaka 1967 na marekebisho yake na 6 ya mwaka 1971.
Katika jitihada hizi Chamijada imetunga sheria za mchezo na kuzifanyia
marekebisho mbalimbali katika mashindano yaliyoandaliwa yakiwemo
Mashindano ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius
K. Nyerere.
Chamijada imezifanyia utafiti kwa miaka minne mfululizo na kuzipeleka kwa
wadau katika manispaa Temeke, Ilala na Kinondoni kwa kuzijadili na kutoa
maoni yao hatimaye kuzipitisha.
Kwasa sheria hii zinakidhi haja ya kuendesha na kuuongoza Mchezo na kutoa
maamuzi bila kuleta athari upande wowote.
Baraza la Michezo la Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wake ambaye ni
Katibu tawala wa Mkoa Ras lilimteua Ndg Monday Likwepa kuwa Mwenyekiti
mtendaji wa Chamijada tangu 2003 na amepewa majukumu matano (5) ya kufanya
na kamati yake nzima kabla ya kuitisha uchaguzi.
|